Tuesday, 9 June 2026
Kenyan Digest

Maafisa wa Polisi wamnasa mshukiwa aliyemuua mpenziwe kisha akamzika

1 min read
Published 30 June 2020

Polisi kaunti ya Kirinyaga wamemkamata jamaa mwenye umri wa miaka 34 anayedaiwa alimuua mpenziwe na kisha kumzika katika boma lake kijiji cha Kianderi.

Naibu Kamishna wa Kirinyaga ya Kati Daniel Ndege aliiambia Citizen Digital kwamba mshukiwa Simon Murimi Wanjohi alikamatwa Jumapili, Juni 28 mtaani Baricho, eneo bunge la Ndia saa tisa asubuhi.

Habari Nyingine: Washukiwa 2 walionaswa kwenye CCTV wakimwibia jamaa kimabavu wakamatwa

Ndege alisema mshukiwa alifumaniwa na babake akichimba shimo bomani mwake Jumanne, Juni 23 lakini alipomuuliza ni la kufanya nini alisema ni la kutupa taka.

Hata hivyo babake aliporejea nyumbani kwa mwanawe siku iliyofuata alikuta shimo hilo limefunikwa na akawaarifu chifu na majirani waliolichimbua.

Habari Nyingine: Serikali yaonya wanasiasa dhidi ya uuzaji wa soko la Mwariro

Muda mfupi baada ya kulichimbua waliona miguu ya mtu na ndiposa wakabaini kuwa jamaa alikuwa amezika mwili.

Mamake marehemu, Beatrice Kabari alisema mwanawe alitoweka Jumatatu.

Polisi waliufukua mwili wa mwanamke huyo Ijumaa na kuupeleka katika hospitali ya Kerugoya ukisubiri kufanyiwa upasuaji.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos