Tuesday, 9 June 2026
Kenyan Digest

Magufuli amfuta kazi mkuu wa wilaya kufuatia madai ya usherati

1 min read
Published 29 June 2020

Rais John Pombe Magufuli amemfuta kazi mkuu wa wilaya kwa madai kuwa amekuwa akizembea kazini na kwamba amekuwa akiwanyemelea wanawake wa wenyewe

Mtela Mwapamba ambaye alikuwa mkuu wa waliya ya Kisarawe alifutwa kazi Jumapili ,Juni 28 na nafasi yake kupewa Mwanana Msumi.

Habari Nyingine: Mchekeshaji wa zamani wa Churchill Show, Kasee aaga dunia

Kwenye video ambayo imeenezwa mitandaoni, Magufuli alisema hataki viongozi ambao hawana uadilifu katika serikali yake ila wale wanaotekeleza wajibu wao.

" Nimesikia mmoja wa wafanyakazi wangu amekosa maadili, kuna madai kuwa amekuwa akiwanyemelea kingono wanawake wa wenyewe, nilimuonya hapo awali lakini hakuonyeka,kwa sasa nafasi hiyo nampea kiongozi mwingine ambaye ataiendesha ipasavyo," Magufuli alisema.

Habari Nyingine: Virusi vya Corona vyaingia Bungeni, Wabunge 6 waambukizwa, mmoja awekwa ICU

Subscribe to watch new videos

Magufuli alimhoji kidogo Mwanana Msumi na kisha kumuamru achukuwe wadhifa huo huku akimweleza Mwapamba kutafuta kazi ya ngazi ya chini.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Subscribe to watch new videos