Connect with us

General News

Papa Francis aanza ziara yake rasmi Afrika – Taifa Leo

Published

on

Papa Francis aanza ziara yake rasmi Afrika – Taifa Leo


Papa Francis aanza ziara yake rasmi Afrika

Na MASHIRIKA

KINSHASA, DRC

PAPA Francis ameanza rasmi ziara yake ya siku sita katika nchi za Afrika.

Kiongozi huyo wa Kanisa la Katoliki amezuru nchi ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo leo Jumatano kama njia ya kuombea amani katika nchi hiyo inayokumbwa na mzozo.

Kanisa Katoliki jijini Kinshasa lilisema kwamba ziara hiyo inalenga maombi maalum ya amani.

Hii ni safari yake ya 40 nje ya nchi tangu alipotawazwa kuwa papa.

Anatarajiwa kukaa katika nchi hiyo hadi Februari 3, atakapoondoka kuelekea Juba na Askofu Mkuu wa Canterbury Justin Welby.



Source link

Comments

comments

Facebook

Trending