[ad_1]
Shambulio jingine Lamu laharibu mashine za ujenzi
Na KALUME KAZUNGU
WAVAMIZI wanaoshukiwa kuwa magaidi Jumapili walivamia kambi ya ujenzi wa barabara eneo la Kwa Omollo, karibu na Bodhei, msituni Boni, Kaunti ya Lamu na kuchoma matingatinga, malori na vifaa vingine vya ujenzi.
Uvamizi huo ulitekelezwa majira ya saa kumi usiku.
Inadaiwa walijigawa makundi matatu kabla ya kuvamia kambi hiyo inayolindwa na wanajeshi wa KDF.
Kamishna wa Kaunti ya Lamu, Bw Irungu Macharia alithibitisha shambulio hilo akasema maafisa wa usalama tayari wameanzisha msako wa waliohusika.
“Walinda usalama wetu walikabiliana nao vilivyo na kuwashinda. Hakuna aliyeuawa wala kujeruhiwa kwenye makabiliano hayo,” akasema.
Shambulio la jana la linajiri wiki moja baada ya kaunti ya Lamu kushuhudia mashambulio yaliyowaacha watu 15, ikiwemo maafisa wanne wa polisi wakiuawa na nyumba zaidi ya kumi zikichomwa kwenye vijiji vya Widho, Juhudi-Ukumi, Mashogoni, Marafa na Bobo-Sunkia.
Next article
Uingereza yadai Putin tayari kuivamia Ukraine
[ad_2]
Source link