Monday, 22 June 2026
Kenyan Digest

Aliyekuwa mtangazaji wa runinga ya K24 Mwanaisha Chidzuga amewaonea hu

1 min read
Published 24 June 2020

Aliyekuwa mtangazaji wa runinga ya K24 Mwanaisha Chidzuga amewaonea huruma zaidi ya wafanyakazi 100 waliofutwa kazi na shirika la utangazaji la Media Max

Chidzuga alifichua kuwa alifutwa kazi mara mbili kutoka kwa mashirika ya utangazaji akiarifiwa kuwa wadhifa wake haukuwa unahitajiki tena katika kampuni.

Kulingana na barua aliyoiandika kwenye mtandao wa Instagram, Chidzuga aliwashawishi mashibiki wake wasiwe wakiabudu sana kazi zao isipokuwa watarajie lolote.

" Marafiki wenzangu, nilijiandikia barua hii mwaka wa 2015 nilipofutwa kazi, nilionelea ni vema nishiriki nanyi ujumbe huu ambao ulibadilisha maisha yangu pakubwa. Ushawishi wangu ni kwamba usiwahi jishikilia sana kwa kampuni na ujihisi uko nyumbani isipokuwa kama una hisa kwa kampuni hiyo," Alisema Chidzuga.

Chidzuga alifutwa kazi mwaka wa 2019 na amekuwa akifanya kila juhudi kuhakisha kwamba anakuwa na maisha bora.

Mrembo huyo aliwatakia heri njema wanahabari zaidi ya 100 waliofutwa kazi katika shirika la Media Max akidai kila mwanadamu lazima awe tayari kwa lolote, liwe baya au nzuri.

Baada ya kufutwa kazi kama mwanahabari, Chidzuga sasa ni mwanzilishi wa hoteli ya Aryanna ambayo inaandaa vyakula vya Kiswahili pekee.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Subscribe to watch new videos