Wednesday, 10 June 2026
Kenyan Digest

Familia yampoteza mtoto wao baada ya kuvamiwa na chui akichunga

1 min read
Published 17 July 2020

- Familia moja Kajiado imempoteza mtoto wao baada ya kushambuliwa na chui

- Mvulana huyo mchanga alikuwa na wenzake malishoni wakati ambapo mnyama huyo alimfumania

- Wakazi wa Kajiado waliteta kuwa wanahangaishwa sana na wanyama wakali wa porini

Huzuni imetanda katika kijiji kimoja Kajiado ya Kati baada ya chui kumtafuna mvulana aliyekuwa akichunga mifugo.

Joshua Marine, mmoja wa jamaa wa familia, alisema kisa hicho kilifanyika wakati mvulana huyo na wenzake walikuwa wakichunga katika eneo la Orgira.

Habari Nyingine: Serikali kuajiri madaktari 20 kutoka Cuba kusaidia kupigana na Covid-19

Chui mweusi kwenye picha ya awali. Familia moja Kajiado inaomboleza kifo cha mvulana wao aliyeshambuliwa na chui. Picha: Citizen
Source: UGC

Marine alisema kisa hicho cha Ijumaa, Julai 17 asubuhi kimeiacha familia yake kwa huzuni kubwa.

Chui aliyehusika aliingia mitini baada ya mashambulizi huku wakazi wakiteta kuwa si mara ya kwanza kwa kisa kama hicho kutokea.

Habari Nyingine: Mtoto wa miezi 5 miongoni mwa wagonjwa 389 wapya wa COVID-19

Wakazi wa Kajiado walisema wamekuwa wakihangaishwa na wanyama pori wakali kama simba na wengine.
Source: UGC

Kamanda wa polisi kaunti ndogo ya Mashuru Ahmed Hillo alidhuibitisha kisa hicho.

Mwili wa mwathiriwa ulipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya rufaa ya Kajiado.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos