KCSE 2021: Jariel Ndeda Obura kutoka Mang’u aibuka mtahiniwa bora kitaifa
NA MWANDISHI WETU
JARIEL Ndeda Obura wa Mang’u High School, ndiye aliyeibuka mwanafunzi bora kitaifa katika Mtihani wa Kitaifa wa Kidato cha Nne KCSE 2021 akiwa na A ya pointi 87.167, matokeo yanaonyesha.
Akitangaza matokeo hayo, Waziri wa Elimu Profesa George Magoha amebainisha kwamba
Jariel Ndeda Obura wa Mang’u High School, ndiye aliyeibuka mwanafunzi bora kitaifa katika Mtihani wa Kitaifa wa Kidato cha Nne KCSE 2021.
Akitangaza matokeo hayo, Waziri wa Elimu Profesa George Magoha amebainisha kwamba ni watahiniwa 826,807 waliofanya KCSE 2021 ikiwa idadi ya juu ukilinganisha na 747,000 waliofanya KCSE 2020. Ni ongezeko la asilimia 10.66.
Aidha, Watahiniwa 1,138 walipata A ambapo 349 ni wa kike nao 789 wakiwa wa kiume.



