Monday, 22 June 2026
Kenyan Digest

Kibaki asifiwa kama aliyeenzi bidii ya maafisa – Taifa Leo

Staff
1 min read
Published 25 April 2022

Kibaki asifiwa kama aliyeenzi bidii ya maafisa

NA WAIKWA MAINA

GAVANA wa Nyandarua, Francis Kimemia amemtaja marehemu Mwai Kibaki kuwa kiongozi aliyezingatia sana utendakazi wa maafisa wakuu serikalini.

Bw Kimemia, ambaye alihudumu kama Mkuu wa Utumishi wa Umma chini ya utawala wa Mzee Kibaki anasema japo Kibaki aliwapa maafisa uhuru wa kufanya kazi bila kuingiliwa, hakupenda watu wazembe.

“Alikuwa akiongoza vikao vya baraza la mawaziri bila kijitabu cha kunukuu hoja zilizojadiliwa, lakini angenasa masuala yote yaliyojadiliwa na maamuzi yaliyofikiwa,” akasema.

Mzee Kibaki aliaga dunia mnamo Ijumaa na atazikwa Jumamosi hii.


About the author