Wednesday, 10 June 2026
Kenyan Digest

Magavana, watu 66 wanasakwa baada ya COVID-19 kupiga hodi ikulu

1 min read
Published 19 June 2020

Viongozi 66 wakiwemo magavana wanasakwa na maafisa wa afya baada ya kutangamana na wafanyakazi wanne wa ikulu waliopatikana na virusi vya COVID- 19 mapema wiki hii

Maafisa wa afya wanataka magavana hao waliohudhuria mkutano wa baraza la mawaziri Juni 10, katika Ikulu wafanyiwe vipimo vya virusi hivyo.

Habari Nyingine: Evariste Ndayishimiye aapishwa kuwa Rais mpya wa Burundi

Magavana waliohudhuria mkutano ikulu kufanyiwa vipimo vya COVID-19
Source: Facebook

Habari Nyingine: Barobaro wa kupenda kubugia atandikwa na mke hadharani

Mkutano huo pia ulihudhuriwa na naibu Rais William Ruto, hata hivyo, haijabainika iwapo Ruto alifanyiwa vipimo ila Rais Uhuru Kenyatta na familia yake hawakupatikana na virusi hivyo.

Imebainika kuwa Rais amefutulia mbali mkutano mwingine wa maafisa wa kaunti ambao ulikuwa ufanyike hii leo Ijumaa, Juni 19, katika ikulu akihofia maambukizi zaidi.

Habari Nyingine: Millicent Omanga achapisha picha za wanawe mtandaoni

Magavana, watu wengine 66 wanasakwa baada ya COVID-19 kupiga hodi ikulu
Source: Facebook

TUKO.co.ke inafahamu kuwa wafanyakazi wanne wa ikulu waliopatikana na COVID-19 wametengwa katika hospitali ya chuo kikuu cha Kenyatta ambapo pia wanapokea matibabu.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Subscribe to watch new videos