Friday, 19 June 2026
Kenyan Digest

Mahakama yamwachilia huru jamaa aliyeingia Ikulu bila idhini

1 min read
Published 27 June 2020

Jamaa aliyengia Ikulu bila Idhini mnamo Juni 19 akinuia kuzungumza na Rais ameachiliwa huru kutokana na matatizo ya kiakili aliyo nayo.

Ripoti kutoka hospitali ya wagonjwa wa akili ya Mathari ambayo iliwasilishwa mbele ya mahakama ilifichua kuwa Luqman Ali Mahmmoud ana matatizo ya kiakili ambayo yalipaswa kushughulikiwa kwa dharura.

Habari Nyingine: Machakos: Hospitali ya Shalom yafungwa baada ya wagonjwa kuangamizwa na coronavirus

Mshukiwa akipelekwa mahakamani baada ya kujaribu kuingia Ikulu. Picha: UGC.
Source: UGC

Hakimu Daniel Ndungi alimwachilia huru Mahmmoud na kumweka mikononi mwa mjombake ambaye alimtaka ampeleke hospitali na kisha amshughulikie ipasavyo kulingana na ripoti ya Daily Nation.

Hata hivyo alionya kuwa iwapo Mahmmoud atarudia kosa hilo basi kesi yake itafufuliwa tena na ataadhibiwa vikali huku mjombake naye akiadhibiwa pia kwa kosa la jinai.

Habari Nyingine: Jalang'o apata kazi mpya baada ya kuondoka Milele FM

Mahmmoud alishtakiwa kwa kuzua vurugu kando na kuingia eneo ambalo linalolindwa na vile vile kukataa kukaguliwa.

Ikulu ya Nairobi ni mojawapo ya maeneo ambayo yako chini ya ulinzi mkali. Picha: State House.
Source: UGC

Mahmmoud ni mtu wa pili kwahi kujaribu kuingia Ikulu kwa nguvu.

Mnamo 2019, wa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia (JKUAT), alishtakiwa baada ya kuruka ua na kuingia Ikulu.

Mwanafunzi huyo aliyetambulika kama Brian Bera alikuwa amejihami kwa kisu wakati akiingia eneo hilo ambalo liko chini ya ulinzi mkali.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos