[ad_1]
Mlalamishi aondoa kesi ya kupinga azma ya Sonko
NA PHILIP MUYANGA
MMOJA wa walalamishi wawili waliotaka aliyekuwa gavana wa Nairobi, Bw Mike Sonko, azuiwe kuwania ugavana Mombasa, amewasilisha ombi kujiondoa kwa kesi hiyo.
Bw Ndoro Kayuga, aliambia Mahakama ya Mombasa kwamba ametambua Bw Sonko aling’olewa mamlakani kisiasa kwa hivyo huenda kesi iliyowasilishwa ni dhaifu kisheria.
Alidai kuwa, uamuzi wake kutaka kujiondoa kwa kesi hiyo haukutokana na vitisho wala kulazimishwa na yeyote.
Next article
Mapigano ya kikabila yaua zaidi ya watu 70
[ad_2]
Source link