Wednesday, 10 June 2026
Kenyan Digest

Mume wa Gladwell Cheruiyot, Isaac Cherogony aangamizwa na COVID-19

1 min read
Published 5 July 2020

Mume wa mwakilishi wa wanawake Kaunti ya Baringo, Gladwell Cheruiyot ameangamizwa na COVID-19.

Isaac Cherogony alipumua pumzi yake ya mwisho usiku wa Jumamosi, Julai 5, katika hospitali moja mjini Eldoret ambapo alikuwa anapokea matibabu baada ya kukumbana na matatizo ya kupumua.

Mbunge huyo pia alifanyiwa vipimo vya virusi hivyo na anasubiri kupokea matokeo yake huku boma lao likifungwa.

Wakati huo huo, ripoti zinadokeza kuwa watu waliokutagusana naye wanafuatiliwa.