Wednesday, 10 June 2026
Kenyan Digest

Picha za kuhuzunisha za halfa ya mazishi ya marehemu Papa Shirandula

1 min read
Published 20 July 2020

Muigizaji maarufu Charles Bukeko, maarufu Papa Shirandula alifariki dunia Jumamosi, Julai 18 mwendo wa saa mbili asubuhi

Papa alikata roho akisuburi kuhudumiwa na madaktari akiwa ndani ya gari lake kama alivyowaambia waombolezaji mkewe mjane Beatrice Ebbie Andega.

Papa alifariki dunia kutokana na virusi vya COVID-19
Source: UGC

Andega aliwashtumu madaktari wa hospitali ya Karen kwa utepetevu kwani anaamini kama mumewe angeshughulikiwa kwa haraka, huenda wangeponya maisha yake.

Awali, Kakake Marehemu alithibitishia vyombo vya habari kuwa Papa aliaga dunia kutokana na virusi vya COVID-19.

Mkewe Papa alisema marehemu alikata roho akisuburi kuhudumiwa na madaktari akiwa ndani ya gari lake
Source: UGC

Shughuli nzima ya mazishi ilifanywa kuambatana na kanuni zilizowekwa na Wizara ya Afya nchini Kenya ili kudhibiti maambukizi ya virusi hivyo.

Wasanii kadhaa waliofanya kazi kwa pamoja na marehemu akiwemo Jackline Nyamide almaarufu Wilbroda walihudhuria mazishi yake.

Shughuli nzima ya mazishi ilifanywa kuambatana na kanuni zilizowekwa na Wizara ya Afya nchini Kenya ili kudhibiti maambukizi ya virusi hivyo.
Source: UGC

Mwili wa Papa ulizikwa saa mbili na dakika 45 asubuhi
Source: UGC

Baada ya ibada fupi ya wafu, waombolezaji waliombwa kutawanyika.
Source: UGC

Papa alizikwa saa mbili na dakika arobaini na tano na kisha waombolezaji wakaombwa kutawanyika.