Wednesday, 17 June 2026
Kenyan Digest

Polisi wafukua mwili wa mwanamke aliyeuawa na kuzikwa na mpenziwe

1 min read
Published 27 June 2020

Mwili wa mwanamke mwenye umri wa miaka 27 aliyezikwa katika kijiji cha Kianderi, eneo bunge la Kirinyaga ya Kati ulifukuliwa Ijumaa, Juni 26 na maafisa wa polisi.

Marehemu aliyetambulika kama Eunice Wambui anaaminika aliuawa na mpenziwe Simon Murimi mwenye umri wa miaka 35.

Habari Nyingine: Jamaa aliyeingia Ikulu bila idhini aachiliwa huru

Mwili wa mwanamke aliyezikwa katika kijiji cha Kianderi wafukuliwa. Picha: Citizen Digital.
Source: UGC

Maafisa wa polisi waliarifiwa na mmoja wa jamaa za mshukiwa kuwa alionekana akichimba kaburi ambalo baadaye alilifunika kwa mchanga.

Mwili wa mwendazake umelazwa katika makafani ya Kerugoya ukisubiri kufanyiwa upasuaji huku polisi wakimsaka mshukiwa ambaye angali mafichoni Citizen Digital iliripoti.

Kiini cha mauaji hayo bado hakijajulikana.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos