Polisi wapeleleza kifo cha kijana katika kampeni za Malala Butere
NA SHABAN MAKOKHA
POLISI wanaendelea kuchunguza kifo cha kijana mmoja ambaye alifariki baada ya kuanguka kutoka kwa gari lililokuwa kwenye msafara wa kampeni za seneta wa Kakamega Cleophas Malala, katika eneobunge la Butere, jana Jumapili.
Kijana huyo, Simeon Odero, anadaiwa alikuwa amening’inia kwenye gari lililokuwa likiendeshwa kwa kasi baada ya Bw Malala, anayelenga kiti cha ugavana, kuhutubia mkutano wa kisiasa katika soko la Sabatia.



