– Ripoti ya BBI inataka nyadhifa za gavana na seneta kufutiliwa mbali
– BBI inapendekeza kaunti hiyo kutawaliwa na Serikali Kuu kinyume na vile imekuwa ikiongozwa na gavana miaka saba iliyopita
– Kaunti ya Nairobi kwa sasa inaongozwa na Gavana Mike Sonko
Huenda Kaunti ya Nairobi ikakosa kuwa na gavana kama kiongozi wake endapo mapendekezo kwenye ripoti ya Jopo Kazi la Maridhiano (BBI), yatapitishwa.
Katika ripoti hiyo iliyokabidhiwa rasmi kwa Rais Uhuru Kenyatta na Kinara wa Upinzani Raila Odinga mnamo Jumanne, Novemba 26, haijata popote kuhusu nyadhifa za gavana na seneta wa jiji kuu nchini.
Hata hivyo, ripoti hiyo badala yake imependekeza kufutiliwa mbali kwa serikali hiyo ya ugatuzi.
Ripoti hiyo iliyotolewa kwa umma na Rais Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila, siku ya Jumatano, Novemba 27, katika ukumbi wa Bomas ambapo wageni zaidi ya 4, 700 walialikwa kuudhuria hafla hiyo.
Kwa sasa Mike Sonko ndiye Gavana wa Nairobi ambapo alichukuwa wadhifa huo kutoka kwa Evans Kidero. Source: UGC
Kaunti ya Nairobi ina wadi 85 zinazowakilishwa na madiwani ambao ni sehemu ya Bunge la Kaunti ya Nairobi pamoja na maeneo bunge 17 yanayowakilishwa na wabunge na maseneta kulingana na gazeti la Taifa Leo.
Kaunti hiyo ambayo kwa sasa inaongozwa na Gavana Mike Sonko aliyechukua usukani Agosti mwaka 2017, kutoka kwa aliyekuwa gavana wa kwanza wa kaunti hiyo Evans Kidero.
Madiwani wakati wa kikao cha awali katika Bunge la Kaunti la Nairobi. Source: UGC
Ripoti ya BBI, imependekeza Nairobi kutunukiwa Hadhi Maalum kama Jiji Kuu nchini na kituo kikuu cha Umoja wa Mataifa na uwakilishaji mwingineo wa kidiplomasia.
Hii inamaana kwamba serikali ya kaunti hiyo huenda sasa ikatawaliwa na Serikali Kuu na wala sio gavana.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 073248269