Connect with us

General News

Bajeti 2019/20: Wapenzi wa mvinyo na sigara kugharamika zaidi ▷ Kenya News

Published

on

[ad_1]

Wapenzi wa mvinyo na sigara watalazimika kugharamika zaidi ili kujiburudisha.

Hii ni baada ya Waziri wa Fedha Henry Rotich kuwasilisha bajeti mbele ya bunge mnamo Alhamisi, Juni 13.

Asilimia 15 ya ushuru imeongezwa kwa bidhaa hizo.

Habari Nyingine: Jamaa awarai wakaazi kumsaidia kumjengea nyumba yatima mlemavu huko Nakuru

Rotich alisema kwamba kuongezwa kwa ushuru hiyo kwa bidhaa hizo itaisaidia serikali kufadhili bajeti yake ya KSh 3 trilioni.

“Napendekeza kuongezwa kwa ushuru kwa sigara na vileo kwa silimia 15. Hii ni kumaanisha kwamba chupa moja ya kiasi cha 750ml ya divai itagharimu KSh 136 ambapo ni KSh 18 ziadi nayo chupa moja ya pombe ya aina ya whiskey ya kiasi cha 750ml itagharimu KSh 182 ambapo ni KSh 24 zaidi.

Pakiti moja ya sigara itagharimu KSh 61 ambapo ni KSh 8 zaidi ya inavyouzwa sasa,” waziri Rotich alifichua.

Kuongezwa kwa ushuru huo aidha kunatarajia kuathiri pakubwa uvutaji wa sigara kwani huenda matumizi ya tobacco yakapungua haswa miongoni mwa vijana.

Habari Nyingine: Wakenya watoa maoni ya kuchekesha kuhusu kukosa kazi licha ya kufika vyuo vikuu

Tangazo hilo aidha linatokea baada ya Shirika la afya duniani WHO kufichua kwamba zaidi ya watu milioni 8 hufariki kila mwaka kutokana na maradhi yanayosababishwa na matumizi ya tobacco huku wakuitoa wito kwa serikali kuwalinda wananchi wake dhidi ya matumizi ya tobacco.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected]; [email protected] au WhatsApp: 0732482690. Tufuate kwa Telegram: Tuko news.

Source: Tuko.co.ke



[ad_2]

Source link

Comments

comments

Facebook

Trending