Tangu zamani wengi wamekua wakifahamishwa kuhusu masomo na kuambiwa kuwa elimu ndio ufunguo wa maisha.
Huu ni msemo na wosia ambao uliwafaa sana wanafunzi katika shule za misingi, sekondari hata vyuoni ambao uliwahimiza kujitahidi kupata alama nzuri ili kuishi maisha bora baadaye.
Habari Nyingine: Washukiwa wa mauaji ya askofu aliyeuwawa Meru wawachiliwa huru
Wakenya watoa maoni yao ya kufurahisha kuhusu kutafuta ajira japo ya kufuzu chuo kikuu. Picha: UGC
Source: Facebook
Habari Nyingine: Kanisa Katoliki kusaidia Uhuru kupiga vita ufisadi
Huku kukiwa na idadi kubwa ya mahafala wanaofuzu kila mwaka changamoto ni idadi ndogo ya nafasi za ajira.
Kufuatia hali hiyo, Wakenya kupitia mtandao wa Facebook wamezua mzaha kuhusu safari zao kutafuta elimu na kujituma sana kupata alama nzuri, lakini mwisho wa siku wanaishi bila ajira huku wengi wakikata tamaa na matumaini.
Wakenya watoa maoni yao kuhusu makosi waliyofuzu katika chuo kikuu. Picha: UGC
Source: Facebook
Habari Nyingine: Duale awasha moto bungeni kwa kudai nafasi ya Wawakilishi wa Kike itaondolewa
Kwa wengine wao kozi walizosomea zlikuwa ngumu zaidi na sasa wanajuta kupoteza muda mwingi, nguvu na pesa kuzisomea.
Mmoja wao anasema kuwa alisomea taaluma ya Bio-Kemia lakini bado hajapata kazi. Huku mwengine akisema alisomea Uhandisi lakini tangu kuhitimue bado anaendelaea kuteseka kutafuta ajira.
Wakenya watoa maoni yao ya kufurahisha kuhusu kutafuta ajira japo ya kufuzu chuo kikuu
Source: Facebook
Kwa wengi, biashara ndio inayowaweka mijini na wala hawakusomea somo la biashara na shahada walizonazo hazijawasaidia hata kidogo.
Odongo Dalton ambaye anasomea Matibabu ya Kinga na ‘toxicology’, anamatumaini siku moja ndoto yake itatimia.
Katika mdahalo huo wa kutaniana kuhusu vyeti, baadhi ya Wakenya wanasema wanapanga kuviuza vyeti hivyo ama kuviteketeza moto.
Hata hivyo, maoni ya wengi yanaelekea kuwa baadhi ya kozi katika vyuo hazifai ama hazina maana yoyote na bora kufutiliwa mbali.
READ ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected]; [email protected] au WhatsApp: 0732482690. Tufuate kwa Telegram: Tuko news.
Source: Tuko