Connect with us

Entertainment

Rapa maarufu Prezzo atangaza kujitosa kwenye ulingo wa kisiasa

Published

on

Rapa maarufu CMB Prezzo ametangaza rasmi kuwa atajitosa kwenye ulingo wa kisiasa katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2022

Ingawa hakutaja ni kiti gani atawania, imeripotiwa kuwa anakimezea mate kiti cha ubunge cha Kibra.

“Ndio nitakuwa debeni mwaka wa 2022 kwa majaliwa ya Mungu, kama niko hai mbona nisijaribu bahati yangu katika siasa,” Prezzo.

Prezzo ameahidi kuleta mabadiliko ambayo wanasiasa wengi huahidi na hawatimizi.

” Lengo langu kuu kujitosa kwenye siasa ni kuleta mabadiliko ambayo wanasiasa wetu wamekuwa wakituahidi na hawatimizi, tayari mimi na kakangu Steve tumeanza kuboresha baadhi ya makazi mtaani Kibra,” Alisema Prezzo.

Rapa huyo ambaye amekuwa katika uliongo wa sanaa kwa zaidi ya miaka 16 ana imani kuwa atakuwa kiongozi wa kila mwananchi.

Wakati wa uchaguzi mdogo Kibra mwaka uliopita, kuliibuka madai kuwa Prezzo angewania kiti cha Kibra kwa tiketi ya chama cha Kalonzo Musyoka cha Wiper Party.

Comments

comments

Trending