Connect with us

General News

ANC yafufua wito Mudavadi awe naibu wa Ruto – Taifa Leo

Published

on

[ad_1]

ANC yafufua wito Mudavadi awe naibu wa Ruto – Taifa Leo

ANC yafufua wito Mudavadi awe naibu wa Ruto

NA WINNIE ATIENO

WANACHAMA wa Amani National Congress (ANC), wamefufua wito kumtaka Naibu Rais William Ruto, kumchagua kinara wao, Bw Musalia Mudavadi, kuwa mgombea mwenza wa urais.

Wakiongozwa mbunge wa Matuga, Bw Kassim Tandaza, ambaye pia ni naibu kiongozi wa ANC, walisema Bw Mudavadi ana tajriba ya kutosha kuwa naibu rais.

Wakiendelea kumpigia debe Bw Ruto Pwani, walisema wana imani ya kuunda serikali kupitia Kenya Kwanza.