– Naibu Rais alikutana na viongozi wa makanisa nyumbani kwake mtaani Karen mnamo Jumanne, Julai 7
– Ruto alisisitiza kwamba ili Kenya ipate ushindi dhidi ya virusi hatari vya corona ni lazima kila Mkenya azingatie maagizo ya serikali ya kudhibiti msambao
– Haya yanajiri baada ya Rais Uhuru kufungua mipaka ya kaunti zilizofungwa kwa takriban miezi miwili ili kudhibiti maambukizi
– Kufikia Jumanne, Julai 7 Kenya ilikuwa imefikisha idadi ya wagonjwa 8,250 wa COVID-19
Naibu Rais William Ruto ametoa wito kwa Wakenya kuchukua jukumu la kibinafsi kukabiliana na msambao wa coronavirus baada ya nchi kufunguliwa.
Akiongea kwake Karen, Nairobi Jumanne, Julai 7 wakati wa mkutano na viongozi wa kanisa kutoka Nyeri, Ruto alisema njia pekee ya kushinda janga hilo ni kuzingatia maagizo yaliyotolewa na serikali.
Naibu Rais akiwahutubia viongozi wa makanisa kwake Karen Jumanne, Julai 7. Picha: William Ruto. Source: Facebook
“Jinsi rais alisema, hili sasa sio jukumu la maafisa wa usalama tena wala miundombinu ya hospitali zetu bali ni mambo ya kawaida sisi kama Wakenya tutajihusisha nayo ambayo yatatusaidia kushinda changamoto hii ambayo imetukumba,” Ruto alisema.
Baadhi ya maagizo yaliyotolewa ni kunawa mikono au kutumia vieuzi, kuzingatia usafi wa hali ya juu katika mazingira, kuepuka misongamanamo ya watu na kuepuka kusafiri ovyo ovyo.
Jumatatu, Julai 6, Rais Uhuru Kenya alifungua mipaka ya kuingia na kutoka kaunti za Nairobi, Mombasa na Marsabit ambayo ilikuwa imefungwa kwa miezi ili kudhibiti msambao wa Covid-19.
Viongozi wa makanisa walioalikwa na DP Ruto kwake mtaani karen wakiwa katika sala. Picha: William Ruto. Source: Facebook
Kiongozi wa taifa aliruhusu makanisa, misikiti na maeneo ya kusali kufunguliwa japo kwa masharti makali ikiwemo waumini 100 tu kwa wakati mmoja.
Hata hivyo idadi ya wale wanaopona pia inazidi kupanda baada ya wagonjwa wengine 90 kuruhusiwa kuondoka hospitalini na kufikisha idadi ya waliopata nafuu 2, 504.
Rais Uhuru Kenya alifungua mipaka ya kuingia na kutoka kaunti zilizofungwa kwa takriban miezi mitatu ili kudhibiti msambao wa Covid-19. Picha: State House Kenya. Source: UGC
Aidha maafa ya watu watu watatu nayo pia ya yaliripotiwa huku idadi sasa ya waliopoteza maisha yao kutokana na virusi hiyo hatari ikifika 167.
Kufikia sasa Wizara ya Afya imepima sampuli 193, 455 tangu kisa cha kwanza cha homa ya corona kutangazwa nchini mwezi Machi.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.