Connect with us

General News

Hakuna wanafunzi kurundikana darasani shule zikifunguliwa

Published

on

[ad_1]

– Magoha alisema wanafunzi watatakiwa kuzingatia sheria ya kutokaribiana ikiwa ni mojawapo ya njia za kudhibiti maambukizi ya virusi vya COVID-19

– Walimu watatakiwa kufika shuleni wiki mbili kabla ya shule kufunguliwa rasmi Septemba 1

– Magoha pia alisema kila mwanafunzi atapewa maski mbili

Waziri wa Elimu Fred Magoha ametangaza kuwa idadi ya juu ya wanafunzi katika darasa moja itakuwa 20 endapo shule zitafunguliwa Septemba.

Magoha alisema serikali inaweka mikakati kabambe ya kuhakikisha kuwa inadhibiti maambukizi ya virusi vya COVID-19.

Habari Nyingine: Mwangi Kiunjuri asajili chama chake

Akizungumza Jumatano, Juni 24 akiwa mjini Kilifi, Magoha alisema walimu watatakiwa kufika shuleni wiki mbili kabla ya shule kufunguliwa rasmi ili wapange ratiba ya jinsi masomo yatakavyoendeshwa.

Waziri huyo pia alisema kila mwanafunzi atapewa maski mbili na atakakiwa kuzingatia sheria ya kutokaribiana.

Habari Nyingine: Wanawake 2 wapigania mwili wa askofu tajiri aliyeaga dunia 2019

“Shule zote pia zitapewa vifaa vya kupima joto mwilini kwa kila mwanafunzi,” Alisema Magoha.

Haya yanajiri siku moja baada ya Magoha kutangaza kuwa kampuni ya Rivatex imepewa kibarua cha kushona zaidi ya maski 22 milioni zitakazosambazwa katika shule zote nchini.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Subscribe to watch new videos



[ad_2]

Source link

Comments

comments

Facebook

Trending