Studio ya runinga ya K24 inayomilikiwa na kampuni ya Mediamax. Mfanyikazi mmoja alithibitishwa kuambukizwwa Covid-19. Source: Depositphotos
“Tungependa kuwajulisha kwamba mfanyikazi kutoka idara ya fedha amethibitishwa kuambukizwa Covid-19 baada ya kuonesha dalili za maradhi hayo. Tayari mfanyikazi huyo huyo ametengwa na anahudumiwa nyumbani kwake,” barua hiyo kutoka kwa Afisa Mkuu Mtendaji Ken Ngaruiya ilisema.
Mnamo Jumatatu Julai, 13, kampuni hiyo ambayo inamiliki runinga ya K24 na kituo cha Milele FM ilifunga afisi zilizoko orofa ya tatu ambazo zinatarajia kupulizwa dawa.
Memo iliyotumiwa wafanyikazi wa Mediamax. Picha: UGC. Source: UGC
Mnamo Jumatatu Julai, 13, kampuni hiyo ambayo inamiliki runinga ya K24 na kituo cha Milele FM ilifunga afisi zilizoko orofa ya tatu ambazo zinatarajia kuoulizwa dawa.
Ngaruiya aliongeza kuwa moango wa kupunguza wafanyikazi katika afisi hiyo tayari umeanzishwa ili kuthibiti maambukizi ya virusi hivyo hatari.
Aidha alisema kuwa tayari kampuni hiyo imeanza kuwasaka watu wote waliotangamana na mfanyikazi huyo.
Wiki jana shirika la Kenya Broadcasting Corporation pia ilitangaza kwamba wafanyikazi wake wawili waliambukizwa virusi vya corona.
Mnamo Jumatatu, Julai 13, Waziri wa Afya Mutahi Kagwe alitangaza watu 189 zaidi waliambukizwa Covid-19 huku visa 12 vya maafa vikiripotiw akatika saa 24 zilizopita.
Visa hivyo vipya vilifikisha idadi ya wagonjwa wa marafdhi hayo nchini kutimia 10,294.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.