– Safaricom itakuwa ikiboresha mfumo wake kuanzia 11.59pm Alhamisi, Julai 9 hadi saa kumi na moja asubuhi Ijumaa, Julai 10
– Wateja hawataweza kupokea kutuma, kupokea pesa wala kununua mjazo wakati wa zoezi hilo ambalo litafanyika kwa saa tano
Kampuni ya mawasiliano ya Safaricom imetangaza kuwa huduma za M-Pesa zitatatizika kwa muda Alhamisi, Julai 9 kati ya saa tano na dakika hamsini na tisa usiku na Julai Ijumaa 10 saa kumi na moja asubuhi.
Kwenye taarifa yake iliyochapishwa mitandaoni Safaricom ilisema huduma zote za M-Pesa ikiwemo ununuzi wa mjazo wa simu zitasitishwa kwa ajili ya kuboresha mfumo wake.
Wateja hawataweza kutuma wala kupokea pesa wakati wa kuboreshwa kwa mfumo huo. Picha: Roberto Muyela/Tuko.co.ke. Source: Original
“Kwa zaidi ya miaka 13, M-PESA imeendelea kubadilisha maisha ya mamilioni ya watu nchini Kenya, kwa kuwaunganisha na fursa mpya kila siku. Ili kuboresha zaidi mabadiliko haya, tunafanya ukarabati wa mfumo wetu mara kwa mara,” taarifa hiyo ilisema.
“Kuhusiana na suala hili, huduma zetu za M-PESA zitakuwa zikikarabatiwa Alhamisi, Julai ,9 2020, kati ya saa tano na dakika hamsini na tisa usiku na saa kumi na moja asubuhi.