Jamaa mwenye umri wa miaka 33 aliyeangamizwa na Covid-19 akipokea matibabu katika hospitali ya Machakos amezikwa kijijini mwao Lemotit, Kipkelion Mashariki.
Marehemu Isaac Sigei, ambaye alikuwa akifanya kazi katika kampuni moja jijini Nairobi alizikwa na maafisa wa huduma ya afya waliozingatia taratibu za kuzuia maambukizi ya Covid-19 na
“Hatujui ni jinsi gani kaka yangu aliambukizwa Covid-19. Tunachojua ni kwamba aliugua na alilazwa kwanza katika hospitali ya Shalom huko Athi River. Lakini, wakati kituo cha afya kilifungwa kwa muda mfupi juu ya mlipuko wa Covid-19, alihamishiwa katika hospitali ya Kaunti ya Machakos aliangamizwa na Covid-19,” alisema.
Kericho ni moja ya kaunti ambayo imechukua hatua dhidi ya Covid-19 kwa kushirikiana na maabara ya Walter Reed Center inayofadhiliwa na Merikani katika kupima sampuli.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.