[ad_1]
Jiungeni kwenye makundi, Achani awarai wanawake
NA WINNIE ATIENO
NAIBU Gavana wa Kwale, Bi Fatuma Achani (pichani) amewarai wanawake kuungana kwa makundi na kuyasajili rasmi.
Alisema hii itawawezesha unufaika na mikopo ya ufadhili wa maendeleo ya kijamii kutoka kwa serikali ya kaunti na ya kitaifa.
Kulingana na Bi Achani, fedha hizo zimesaidia makundi ya wanawake kujikuza hasa katika biashara zao na wengine wengi wanalengwa kunufaika.
Alisema hayo huku anapoendelea kujipigia debe kwa ugavana katika uchaguzi ujao, akieneza sera ya kuleta maendeleo vijijini.
[ad_2]
Source link