Kiranja wa wachache katika Bunge la Kitaifa Junet Mohamed amepuuzilia mbali mbali madai kuwa, chama cha ODM kinapanga kujiondoa kwenye salamu ya maridhiano kati ya Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa Upinzani Raila Odinga.
Kiranja wa wachache katika Bunge la Kitaifa Junet Mohamed akiwa na wanasiasa wenzake kutoka chama cha ODM katika picha ya zamani. Picha: Nation Source: Facebook
Kulingana na Junet, wanasiasa kutoka mrengo wa Tangatanga katika chama tawala cha Jubilee ndio wanaoeneza uvumi kuhusu ujumbe uliosambaa mitandaoni ukidai alimkemea Katibu Mkuu wa Chama cha Jubilee Raphael Tuju na Naibu Mwenyekiti wa cama hicho David Murathe.
“Hali ya kuhangaika katika Tangatanga ni mbaya zaidi. Hizi jumbe FEKI wataziandikia wanasiasa wangapi? Shika adabu yako Ndungu Wainaina kuwa mtu mzima, hufai kuwa unaandika vitu vya aina hii,” mbunge huyo alisema kupitia Twitter
Junet, ambaye ni mmoja wa wandani wa Odinga, hata hivyo hakuzungumzia mgogoro unaodaiwa kuwapo kati ya wabunge wa ODM na Jubilee kuhusu mchakato wa BBI.
Mnamo Jumatatu, Mwenyekiti wa ODM ambaye pia ni kiongozi wa wachache katika bunge la kitaifa John Mbadi aliwalaumu viongozi wa Jubilee katika alichotaja ni kukosa kuchukulia mchakato huo kuwa wenye uzito.
Rais Uhuru Kenyatta, Naibu Rais William Ruto na KIongozi wa ODM Raila Odinga wakati wa uzinduzi wa ripoti ya BBI katika ukumbi wa Bomas Of Kenya, Novemba, 2019. Picha: The Star Source: UGC
Matamshi ya Mbadi yalijiri baada ya Chama cha Jubilee kusisitiza ni lazima marafiki wa Naibu Rais William Ruto kujumuiswa kwa wingi katika kamati itakayoshughulikia sheria zinazohusiana na BBI.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.