-Marehemu anasemekana kupigwa risasi na kuawa na polisi mmoja kutoka kituo hicho baada ya kugombania kitakasa mkono
-Mamia ya wandamanaji walikusanyika huku wakiimba wimbo wa vita na kutaka haki kabla ya kutekeketeza kituo hicho
– Wakazi walitumia chochote kilichokuwa mbele yao kuharibu kituo hicho
Halaiki kubwa ya watu wenye hamaki katika kaunti ya Kisii waliandamana kukashifu mauaji ya mfanyabiashara mmoja siku ya Jumapili, Julai 5, na kushuhudiwa wakiteketeza Kituo cha Polisi cha Rioma.
Marehemu anasemekana kupigwa risasi na kuawa na polisi mmoja kutoka kituo hicho baada ya kugombania kitakasa mkono.
Wakazi walitumia chochote kilichokuwa mbele yao kuharibu kituo hicho licha ya kuzingirwa na wingu kubwa la moshi huku wakimtaka afisa aliyetekeleza mauaji hayo akamatwe na kushtakiwa kwa mauaji.
Kisa hicho cha Kisii kinakujia yapata mwezi mmoja baada ya kingine kushuhudiwa katika Kituo cha Polisi cha Naivasha.
Katika tukio hilo la Naivasha, maafisa wanane wa polisi walinusurika kifo baada ya kambi yao kuteketezwa eneo la Naivasha wakati wa mandamano ya kukashifu udhalimu wa polisi.
Inaaminika kuwa wakazi wa eneo hilo wamekuwa wakilalamikia kudhulumiwa na maafisa wa polisi wa kambi hiyo jambo ambalo linasemekana lilichangia tukio hilo.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.