Maabara ya hospitali ya Lang’ata ilifungwa ghafla Jumatano, Julai 8 kwa madai kuwa imekuwa ikifanya vipimo na kutoa matokeo feki ya virusi vya covid-19
Maafisa wa bodi ya kusimamia maabara nchini (KMLTTB), walifanya msako mkali katika hospitali hiyo na kubaini kuwa haikuwa na vifaa vya kupimia ugonjwa huo.
Vile vile, imebainika kuwa maabara hiyo imekuwa ikiwalipisha wagonjwa KSh 5,500 kwa ajili ya vipimo vya virusi hivyo na kisha sampo zinapelekwa KEMRI kwa majaribio.
Maabara ya hospitali ya Lang’ata yafungwa kwa kufanya vipimo feki vya COVID-19 Source: UGC
‘’Kilichotufanya kufunga maabara hiya ni kuwa haina vifaa vya kutumika katika kupima virusi vya corona, hivyo inamaamisha wamekuwa wakiwahadaa wananchi na kuweka maisha yao hatarini,” Alisema Patrick Patrick Kisabei ambaye ni afisa mkuu mtendaji wa bodi hiyo.