Connect with us

General News

Mfanyakazi wa shamba ang’oa mboga kunyimwa mshahara

Published

on

[ad_1]

Mkulima wa eneo la Kianie, Machakos anakadiria hasara baada ya mfanyakazi wake kuingia shambani ka kung’oa mboga zote alipokosa kumlipa mshahara wa miezi mitatu.

Duru zinaarifu kwamba baada ya lofa kumsababishia mwajiri wake hasara hiyo alitoweka.

Habari Nyingine: Kajiado: Chui wamtafuna kijana aliyekuwa akichunga mifugo

Mfanyikazi wa shamba ang'oa mboga kwa kunyimwa mshahara

Mboga shambani. Picha: TUKO.co.ke.
Source: Original

Kwa mujibu wa Taifa Leo, mfanyakazi huyo anasemekana alitambulika na wengi kwa bidii yake kazini lakini mwajiri wake alikuwa akimpuuza kila mara alipoitisha mshahara wake.

Hata hivyo, jamaa alipochoka hudai hela zake alizua kioja alipofika kwa mdosi wake akafululizi hadi shambani na kung’oa mboga zote alizopanda kabla ya kuchukua virago na kuondoka.

Habari Nyingine: Seneta Sakaja alala ndani baada ya kunaswa akibugia pombe usiku

Inasemekana nusra mdosi wake adondokwe na machozi baada ya kuarifiwa kilichitokea kwani alitumia maelfu ya pesa kwenye mradi wa upanzi wa mboga.

Hata hivyo alibaki kunyoshewa kidole cha lawana na wenyeji waliomsuta kwa mazoea yake ya kutolipa wafanyakazi wake.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos



[ad_2]

Source link

Comments

comments

Facebook

Trending