Nyumba za kupangisha. Mpangaji mtaani Kawangware azua kioja kuhepa na mke wa ‘caretaker’. Picha: UGC. Source: UGC
Kulingana na Taifa Leo, kijogoo alikuwa katika uhusiano wa kimapenzi kisiri na kidosho huyo ijapokuwa baadhi ya wapangaji walishuku na hata kumnong’onezea mumewe.
Hata hivyo siku ya kisanga ‘caretaker’ huyo alikuwa ameenda kudai kodi kutoka kwa wapangaji waliokuwa wakiishi nyumba zingine za mwajiri wake wakati aloporeja na kupata mlango wake ukiwa wazi.
“Hii nyumba leo imenyamaza hivi kwani watu walienda wapi? Unemuona mke wangu?” jamaa alisikika akimuuliza jirani.
Jamaa alijaribu kumtafuta mkewe kwa simu akamkosa na alipochungulia nyumba ya barobaro aliyetoweka na mkewe alipigw ana butwaa kuona iliachwa wazi bila chochote ndani.
Penyenye zinasema ‘caretaker’ alianza kutokwa na kijasho jembamba. Wapangaji kwenye ploti walianza kupata habari kuhusu kilichompata msimamizi wa ploti yao.
“Mkeo nilimuona na begi kubwa akienda. Jamaa anayeishi kwenye chumba kile alikuwa amembebea begi yake ndogo ya mkononi,” mpangaji mmoja alisikika akisema.
“Wewe tulikupasha habari kuhusu uhusiano wa mkeo na huyo jamaa ukapinga. Mkeo ameenda,” sauti nyingine ya mpangaji ilisikika.
‘Caretaker’ alishindwa aanzie wapi.
“Tafuta mke mwingine uoe. Huyo ameenda,” alielezwa.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.