Connect with us

General News

Mtu ‘hakubali na jambo’ hulikubali jambo fulani – Taifa Leo

Published

on

[ad_1]

Mtu ‘hakubali na jambo’ hulikubali jambo fulani – Taifa Leo

NDIVYO SIVYO: Mtu ‘hakubali na jambo’ hulikubali jambo fulani

NA ENOCK NYARIKI

KATIKA makala yaliyotangulia, tulieleza kwamba mojawapo ya sababu ambazo yamkini huwafanya watu kutumia kauli ‘kataa na’ kwa maana ya kutotaka kitu fulani ni tafsiri ya moja kwa moja ya kauli hiyo kutoka katika lugha zao za kwanza.

Tulitoa mfano wa lugha za Kikikuyu na Kikisii ambapo ‘na’ hutumiwa kama neno la kusisitiza na kuashiria.

Hoja nyingine ambayo inafungamana na tafsiri ya moja kwa moja ya kauli hiyo’ ni ukuruba wa kimatumizi wa maneno ‘acha’, ‘kataa’ na ‘tengana’.

Katika miktadha fulani, lugha hizo huyatumia maneno hayo matatu kwa njia sawa. Yaani, kauli ‘achana na wizi’, *‘kataana na wizi’ na ‘tengana na wizi’ huchukuliwa kuwa na maana sawa.

Jambo la pili ambalo yamkini huwafanya watu kutumia kauli ‘kataa na’ katika mawasiliano ni kutumiwa kwa ‘na’ na neno jingine ambalo ni kinyume cha kataa.

Watu husema ‘kubaliana na’ wakiwa na maana ya kuunga mkono ama kuvutiwa na hoja au pendekezo.

Madhali, kunao msemo ‘kubaliana na’ katika lugha ya Kiswahili, watu wengine hudhani kwamba kinyume cha msemo huo ni ‘kataana na’ au ‘kataa na’; jambo ambalo si kweli!

‘Kubaliana na’ ni msemo ambao hauna maana ya moja kwa moja ya ‘kubali’.

Neno kubali lina maana mbalimbali ila nitataja zile ambazo zinahusiana na makala haya: afiki jambo, sema ndio, ridhika, kiri n.k.

Ni muhimu kufahamu kuwa ‘mtu hukubali jambo’ wala ‘hakubali na jambo’.

MAKALA YATAENDELEA

[ad_2]

Source link

Comments

comments

Trending