Connect with us

General News

Mwigizaji wa Mother- In- Law, apona baada ya kuugua kwa muda mrefu

Published

on

[ad_1]

Mtangazaji wa redio ya Hot 96 na mwigizaji nyota katika kipindi cha Mother In- Law Andrew Muthure almaarufu Mustafa amepata nafuu baada ya kuugua kwa muda mrefu

Mustafa alitangaza kurejea kwake kwenye runinga kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram na kumshukuru Mungu kwa uhai na mashabiki waliomuombea afueni ya haraka.

TUKO.co.ke inafahamu kuwa Mustafa alikuwa akipokea matibabu katika hospitali ya St Pauls hapa jiji Nairobi.

” Nimerejea kwa kishindo, niko buheri wa afya na nafurahia sana,” Alisema Mustafa akionekana kuwa mwingi wa furaha.

Hata hivyo , haijabainika msanii huyo alikuwa akiugua ugonjwa upi lakini familia yake inafurahia kuona akiwa buheri wa afya.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Subscribe to watch new videos



[ad_2]

Source link

Comments

comments

Facebook

Trending