– Ngunjiri alidai safari ya Joho na Junet ilitumia KSh 30M kuenda Dubai kumuona Baba hospitali
– Alisema hayo ni matumizi mabaya wakati ambapo mamia ya vijana wanateseka mitaani na zingetumika kuleta miradi ya maendeleo
– Aidha baadhi ya wanasiasa wanadai pesa hizo zilitoka katika mfuko wa mlipa ushuru
Mbunge wa Bahati Kimani Ngunjiri amesema Gavana wa Mombasa Hassan Joho na mbunge wa Suna Mashariki walitumia KSh 30M kukodisha ndege ya kuenda kumuona Raila Odinga Dubai.
Wawili hao waliondoka humu nchini Alhamisi, Julai 9 kusafiri hadi Dubai wakitumia ndege ya kifahari.
Mbunge Kimani Ngunjiri. Ngunjiri amedai Hassan Joho na Junet Mohammed walitumia KSh 30M kuenda kumuona Raila Odinga Dubai. Picha: Kimani Ngunjiri Source: UGC
Ngunjiri alisema hatua ya wawili hao ni kama madharau kwa Wakenya wambao wanateseka kipindi hiki cha Coronavirus.
“Junet na Gavna wa Mombasa Hassan Joho walitumia KSh 30M kuenda tu kumuona mgonjwa na kurudi. Na ikikadiriwa vizuri itafika hata bilioni. Kwa nini tutumie hizi pesa kwa njia hii? alisema Mbunge huyo.
“Kama tungeaambiwa fedha hizo zilitumika kulipia bili ya hospitali ya Raila tungeelewa lakini si kuonyeshwa zimetumika kulipia watu wawili safari ya kifahari,” aliongeza
Habari Nyingine:
Ngunjiri alisema fedha hizo zilifaa kutumika katika kuinua maisha ya vijana humu nchini katika kuzindua miradi ya maendeleo.
Safari ya wanasiasa hao imekuwa ikikosolewa na wanasiasa wengine akiwemo aliyekuwa seneta wa Kakamega Bonny Khalwale.
“Ndege ya kipekee kuenda kumtembelea mgonjwa Dubai. Hivi ndio ushuru wenu unatumika,” alisema Khalwale.