[ad_1]
Mtangazaji maarufu wa runinga ya KTN Marry Kilobi anasherehekea siku yake ya kuzaliwa hii leo Alhamisi, Julai 16
Mumewe ambaye ni katibu mkuu wa chama cha wafanyakazi (COTU), Francis Atwoli alikuwa wa kwanza kumtumia ujumbe mtamu wenye heri njema na kumtakia maisha marefu.
Habari Nyingine: Ni Raila pekee atamuweza Ruto 2022, mchanganuzi Herman Manyora asema
Maneno matamu ya Atwoli kwa mkewe Mary Kilobi siku yake ya kuzaliwa
Source: UGC
Atwoli alisema anamshukuru Mungu kwa kumleta ‘Maria’ kama anavyomuita mwenyewe katika maisha yake.
” Heri njema siku yako ya kuzwaliwa Maria, hebu na Mungu akulinde na akupe maisha marefu ili uweze kuendelea kunilinda mimi pamoja na familia yangu,” Alisema Atwoli.
Habari Nyingine: Magazeti ya Alhamisi, Julai 16: Mbunge, majaji wawili ni miongoni waliougua COVID-19 kwa siku 60
” Wewe ni wa maana sana maishani mwangu na kuombea baraka tele kutoka kwa Mwenyezi Mungu,” Atwoli aliongezea.
Wakenya mitandani pia wamemtumia Kilobi jumbe za heri njema na maisha marefu.
READ ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
[ad_2]
Source link