General News
Village Girl ajitosa kikamilifu katika uigizaji
Published
4 years agoon

TANGU akiwa mtoto alidhamiria kuhitimu kuwa mwanasheria, lakini elimu ilimpiga chenga na ndoto hiyo kuyeyuka.
Lena Mutindi Mailu maarufu Village Girl ni mmoja kati ya akina dada wengi tu ambao hujipata katika taaluma tofauti kinyume na matarajio yao.
Binti huyu aliyezaliwa mwaka 1992 ni mfanyabiasharaandishi wa filamu pia mwigizaji anayekuja.
”Ingawa nilitamani kuwa wakili baadaye nilivutiwa na masuala ya uigizaji baada ya kutazama kipindi cha ‘Zora’ ambacho hupeperushwa kupitia Citizen TV,” alisema na kuongeza kuwa ana imani anatosha mboga pia anaamini ipo siku atakubalika na kuibuka staa katika tasnia ya uigizaji.
Anasema uigizaji wake Sarah Hassan ulimtia motisha zaidi kujiunga na ulingo huo mwaka 2019. Kipindi hicho alianza kushiriki reality show kilichokuwa kinarushwa kupitia Maishamagic.
Kisura huyu anajivunia kushiriki filamu kama ‘Njoro wa Uber,’ ‘Zora’ ‘Antiboss,’ na ‘Maria,’ kati ya nyingi nyinginezo.
Anadokeza kuwa kamwe hawezi kuweka katika kaburi la sahau mwaka 2020 aliposhiriki filamu iitwayo 40 Sticks iliyopeperushwa kupitia Netflix. Pia amefanya kazi na kundi la Waite Empire ambalo hukuza waigizaji wanaoibukia.
“‘Ninachukua muda huu nishukuru wakurungezi wa kikundi hicho kwa kukuza kipaji changu,” alisema na kuongeza waliwatangulia wanapaswa kuwa na moyo kama huo. Kisura huyu anasema anahisi pia amepania kuwa kati ya wanadada watakaofanikiwa Kenya kutinga upeo wa kimataifa katika sekta ya uigizaji.
Katika uigizaji wake anasema kwamba kamwe hawezi kuweka katika kaburi la sahau kipindi cha ‘Zora’ maana huwa na mpangilio wa kimataifa.
Binti huyo analenga kufuata nyayo zake mwigizaji wa kimataifa Meryl Streep mzawa wa Marekani maana kazi zake humchochea kutolengeza kamba katika masauala ya uigizaji. Mwigizaji huyo anajivunia kuteuliwa kuwania tuzo za Oscar mara kadhaa huku akishinda tuzo nne:Oscar mara tatu (1980, 1983, 2012 )na Golden Gloves mara moja mwaka 2017. Aidha ameteuliwa mara kadhaa kuwania tuzo ya BAFTA Awards anakojivunia kushinda mara moja.
Afrika angependa kufanya kazi na waigizaji kama Masasa Mbangeni mzawa wa Afrika pia Sindy Amande raia wa Cameroon wanaojivunia kushiriki filamu kama ‘Scandal,’ na ‘A man for the weekend,’ mtawalia.
Anashauri wenzie kuwa hakuna njia ya mkato bali wawe na subira pia wabunifu na kumweka Mola kwa kila jambo wanalofanya. ”Ningependa kuwaambia kuwa hakuna kizuri uja rahisi lazima binadamu waze na kuwazua bila kulaza damu mzigoni,” akasema.
Wakenya wengi hupenda kuzatama filamu za kigeni ikiwamo za kinigeria (Nolly wood). ”Hakuna binadamu asiyependa kutazama utamaduni wa mataifa mengine. Kasumba hiyo imefanya wengi wetu kuvutiwa na filamu za Nigeria maana hufanyiwa katika madhari ya kuvutia,” akasema.
Kando na uigizaji amepania kujibidiisha katika uandishi wa filamu kuhakikisha ametambulika pia anawazia kumiliki brandi yake na kujitwika jukumu la kulea waigizaji chipukizi wavulana na wasichana. Kuhusu changamoto anashikilia mtoto wa kike hukubana na pandashuka kibao.
PICHA NA JOHN KIMWERE
Lena Mutindi Mailu maarufu Village Girl mwigizaji anayekuja anayepania makubwa miaka ijayo.Na JOHN KIMWERE
TANGIA akiwa mtoto alidhamiria kuhitimu kuwa mwanasheria, lakini elimu ilimpiga chenga na ndoto hiyo kuyeyuka. Lena Mutindi Mailu maarufu Village Girl ni kati ya wana dada wengi tu ambao hujipata katika taaluma tofauti kinyume na matarajio yao. Binti huyu aliyezaliwa mwaka 1992 ni mwana biashara, mwandishi wa filamu pia mwigizaji anayekuja. ”Ingawa nilitamani kuwa wakili baadaye nilivutiwa na masuala ya uigizaji baada ya kutazama kipindi cha Zora ambacho hupeperushwa kupitia Citizen TV,” alisema na kuongeza kuwa ana imani anatosha mboga pia anaamini ipo siku atakubalika na kuibuka staa katika tasnia ya uigizaji. Anasema uigizaji wake Sarah Hassan
ulimtia motisha zaidi kujiunga na ulingo huo mwaka 2019. Kipindi hicho alianza kushiriki reality show kilichokuwa kinarushwa kupitia Maishamagic.
Kisura huyu anajivunia kushiriki filamu kama ‘Njoro wa Uber’, ‘Zora’, ‘Antiboss’ na ‘Maria,’ kati ya nyingine.

Anadokeza kuwa kamwe hawezi kuweka katika kaburi la sahau mwaka 2020 aliposhiriki filamu iitwayo ’40 Sticks’ iliyopeperushwa kupitia Netflix.
Pia amefanya kazi na kundi la Waite Empire ambalo hukuza waigizaji wanaoibukia.
”Nachukua muda huu nishukuru wakurungezi wa kikundi hicho kwa kukuza kipaji changu,” anasema na kuongeza waliowatangulia wanapaswa kuwa na moyo kama huo.
Kisura huyu anasema anahisi pia amepania kuwa kati ya akina dada watakaofanikiwa Kenya kutinga upeo wa kimataifa katika sekta ya uigizaji.
Katika uigizaji wake anasema kwamba kamwe hawezi kuweka katika kaburi la sahau kipindi cha ‘Zora’ maana huwa na mpangilio wa kimataifa.
Binti huyo analenga kufuata nyayo zake mwigizaji wa kimataifa Meryl Streep mzawa wa Marekani maana kazi zake humchochea kutolengeza kamba katika masauala ya uigizaji. Mwigizaji huyo anajivunia kuteuliwa kuwania tuzo za Oscar mara kadhaa huku akishinda tuzo nne:Oscar mara tatu (1980, 1983, 2012) na Golden Gloves mara moja mwaka 2017. Aidha ameteuliwa mara kadhaa kuwania tuzo ya BAFTA Awards anakojivunia kushinda mara moja.
Afrika angependa kufanya kazi na waigizaji kama Masasa Mbangeni mzawa wa Afrika pia Sindy Amande raia wa Cameroon wanaojivunia kushiriki filamu kama ‘Scandal,’ na ‘A man for the weekend,’ mtawalia.
Anashauri wenzie kuwa hakuna njia ya mkato bali wawe na subira pia wabunifu na kumweka Mola kwa kila jambo wanalofanya. ”Ningependa kuwaambia kuwa hakuna kizuri uja rahisi lazima binadamu waze na kuwazua bila kulaza damu mzigoni,” akasema.
Wakenya wengi hupenda kuzatama filamu za kigeni ikiwamo za kinigeria (Nollywood).

”Hakuna binadamu asiyependa kutazama utamaduni wa mataifa mengine. Kasumba hiyo imefanya wengi wetu kuvutiwa na filamu za Nigeria maana hufanyiwa katika madhari ya kuvutia,” akasema.
Kando na uigizaji amepania kujibidiisha katika uandishi wa filamu kuhakikisha ametambulika pia anawazia kumiliki brandi yake na kujitwika jukumu la kulea waigizaji chipukizi wavulana na wasichana. Kuhusu changamoto anashikilia mtoto wa kike hukubana na pandashuka kibao.
[ad_2]
Comments
The Kenyan Digest Team
You may like
Xiaomi Unveils REDMI Note 15 Series: REDMI Titan Durability Meets Advanced Imaging
SportyBet’s 1UP Early Win Is a Game-Changer for Kenyan Punters in 2026
Evidence-Based Study Strategies for Academic Success in Higher Education
Securing Scholarships for International Study: A Comprehensive Guide for Students
Paul Ndung’u Bankruptcy Exposes a Stunning Fall After SportPesa Court Defeat
Arsenal vs Manchester United Prediction: Betting Tips, Odds, and Match Preview
EXPOSED: Court Filings Show How Cs Mbadi, Watanga and Nyawanda Approved Sh5.5 Billion Illegal Rice Imports
The 2027 Expiry Date: Why Moses Omondi’s Term Will Be Short
The Two Faces of Opiyo Wandayi: The ‘Watcher’ Who Now Uses Luo Votes While Kenyans Pay the Price