Connect with us

General News

Wafanyakazi wawili wa shirika la KBC wakutwa na virusi vya COVID-19

Published

on

[ad_1]

Wafanyakazi wawili wa shirika la utangazaji la KBC wamepatikana na virusi hatari vya COVID- 19

Habari hii ilitangazwa na mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo Naim Bilal siku ya Jumatatu, Julai 7.

Habari Nyingine: Safari za ndege kuingia na kutoka nchini kurejelea huduma kawaida – Uhuru l

” Imebainika kuwa wafanyakazi wetu 2 wamepatikana na virusi vya COVID-19, hata hivyo, tumekuwa tukizingatia masharti yaliowekwa na wizara ya afya ya kudhibhiti maambukizi ya virusi hivyo, ” Alisema Bilal.

Bilal pia aliwashauri wale ambao wametangamana na wagonjwa hao wawili kujitokeza ili wafanyiwe vipimo vya COVID-19 au wajiweke karatini.

Vile vile, wale ambao wanajihisi wagonjwa wameshauriwa kutafuta huduma za daktari iwapo wanahisi dalili zozote za magonjwa yoyote.

Habari Nyingine: Moses Kuria asababisha kipindi cha runinga kukatizwa ghafla kwa matamshi yake tata

Haya yanajiri huku Kenya ikiwa imerekodi visa 7,400 vya maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa COVID-19 na vifo 160 kuripotiwa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Subscribe to watch new videos



[ad_2]

Source link

Comments

comments

Trending