Connect with us

Entertainment

Pasta afumaniwa akishiriki ufuska na kondoo

Published

on

Mchungaji aliyefumaniwa akila uroda na mke wa muumini wake aliponea kifo kwa tundu la sindano.

Muumini huyo, Joseph alirejea nyumbani mapema kutoka kazini na kumpata pasta akipakua asali ya mkewe kitandani mwao jinsi Kenyan Digest ilivyoripoti.

Kakamega: Pasta afumaniwa akipakua asali ya mke wa muumini wake

Wakazi wenye hamaki walimsuta mchungaji huyo kwa kuhusika katika kisa hicho cha aibu.

Katika patashika hiyo, pasta huyo wa kanisa la Solid Rock for Jesus Christ alitoroka kwa miguu na kuwacha nyuma pikipiki yake na baadhi ya nguo zake.

Kisa hicho kiliwaudhi wakazi wa kijiji cha Elukho, eneo bunge la Lurambi, kaunti ya Kakamega ambao walimsuta mchungaji huyo wakimtaja kama mtu asiyemcha Mungu.

Chifu wa eneo hilo Alex Mutende alilaani kitendo cha wawili hao na kufichua kwamba polisi wameanzisha uchunguzi.

Aliongeza kuwa maafisa hao pia wameizuilia pikipiki ya mchungaji huyo kando na kuchukua nguo alizoacha kwa mama huyo akikimbilia usalama wake.

Wenyeji waliitaka familia ya mchungaji huyo kuomba msamaha kwa kosa hilo na kumkabidhi Josephat ng’ombe na mbuzi kupitia kwa chifu.

Hata hivyo, mlalamishi aliyejuwa na hamaki aliapa kutomsamehe mkewe licha yao kuwa na watoto watatu.

Comments

comments

Facebook

Trending