– Aliyekuwa dereva wa Kidero sasa amelazimika kuchuuza parachichi baada ya mwanasiasa huyo kushindwa 2017
– Alisema alikuwa amemwahidi kuanzisha biashara lakini baadaye akazima simu na kumlazimu kutafuta njia ya kujikimu
– Amewataka vijana wasichague kazi ili wapange kujiajiri hata kama mapato yatakuwa ni madogo
Damon Osawa ni mmoja wa watu ambao kwa sasa wanajua maana halisi ya msemo mambo hubadilika.
Kwake, hata hivyo, ni mabadiliko mabaya kwani ameshuka kutoka kwa barobaro aliyevaa suti na kusimama wima hadi kuwa wa kupinda kiuno kuuza parachichi.
Habari Nyingine: Ijumaa Julai 10: Watu 473 zaidi wapatwa na coronavirus
Aliyekuwa dereva wake Evan Kidero, Doman Osawa, sasa ni muuzaji parachichi.
Source: Original
Osawa alikuwa mtu tajika kwani alihudumu kama dereva wa aliyekuwa gavana wa Nairobi Evan Kidero.
Alifanya kazi pia kama afisa wa mipango kuhusu masuala ya vijana kwenye afisi ya Kidero.
Lakini hayo ni yaliyopita kwani baada ya Kidero kupokea kichapo kwenye debe 2017 mambo yalimuendea mrama kijana Osawa.
Habari Nyingine: Baba afurahia kukutana na vijana wake Gavana Joho, Junet
Alisimulia kuwa mambo yaligeuka pakubwa kwenye maisha yake na kumfanya kuhangaika mitaani bila kuamini kushuka kwake kimaisha.
Kufikia Januari 2020, aliamua kuingia kwenye biashara bila ya haya kuwa alikuwa amepanda ngazi kimaisha na ndipo akaanza kuuza parachichi.
Habari Nyingine: Ngome ya kisiasa ya Rais Uhuru Kenyatta yaendelea kupasuka
Doman Osawa alikuwa dereva wa Evans Kidero kuanzia 2013 mpaka 2017. Picha: Damon Osawa
Source: Facebook
“Niliamua nifanye hii biashara kujitafutia shilingi zaidi na nipate wazo lipya,”alisema.
Akiongea na TUKO.co.ke, alisema kufanya kazi kwake na Kidero kulimpa ufuasi mkubwa mtandaoni ambapo anatumia kunadi bidhaa zake.
Marafiki aliopata kwenye jumba la City Hall, wakiwemo MCAs, wamekuwa baadhi ya wateja wake sugu.
Habari Nyingine: Daktari Mkenya afariki dunia kutokana na COVID-19
Damon Osawa amekuwa akiwauzia waliokuwa MCAs rafiki wake katika City Hall parachichi.
Source: Original
Alisema mara ya mwisho kuzungumza na Kidero alimwahidi kumsaidia kuanzisha biashara lakini mawasiliano yalifika kikomo.
“Tuliongea baada ya 2017 na akaniahidi kunisaidia nianzishe biashara lakini mawasiliano yakafika kikomo mwanzoni mwa 2018 bila kujua sababu,” alisema.
“Biashara hii inanipa kitu kidogo na ninajivunia kwa sababu ni yangu. Kama vijana, wacheni tuamue kujiajiri,” alisema.
READ ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Subscribe to watch new videos