Connect with us

General News

Wali na nyama – Taifa Leo

Published

on

[ad_1]

Wali na nyama – Taifa Leo

MAPISHI KIKWETU: Wali na nyama

NA MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 15

Muda wa mapishi: Dakika 30

Walaji: 4

Vinavyohitajika kwa wali

  • mchele kilo ½
  • tui la nazi kikombe 1
  • maji mara mbili ya kiasi cha mchele
  • chumvi

Maelekezo

Osha mchele.

Weka mchele jikoni na ongeza chumvi. Acha mchele hadi uanze kuchemka.

Ukishaanza kuchemka, ongeza tui la nazi. Usikoroge.

Acha mchanganyiko uive taratibu kwa dakika 10.

Punguza moto na uache wali uive hadi maji yakauke.

Epua.

Vinavyohitajika kwa nyama

nyama kilo 1

vitunguu maji 2

vitunguu saumu 2

tangawizi 1

nyanya 4

mafuta ya kupikia

chumvi kijiko 1

pilipili mboga 1

Maelekezo

Menya vitunguu na pilipili mboga na ukate viwe vipande vyembamba sana.

Menya nyanya na tangawizi kisha ukatekate.

Twanga vitunguu saumu kisha bandika sufuria ya kupikia jikoni.

Weka nyama na anza kukoroga ishikilie kwenye sufuria na ikauke.

Weka kitunguu maji huku ukiendelea kukoroga kwa muda wa dakika 10.

Ongeza kitunguu saumu na tangawiizi huku ukikoroga.

Weka mafuta ya kupikia kisha weka pilipili mboga. Ongeza chumvi kidogo. Endelea kukoroga.

Weka nyanya, koroga na funika sufuria kisha uache kwa dakika 10.

Pakua na ufurahie.