– Akothee alitangaza kuwazawadi mashabiki wake bora kwenye YouTube mwaka huu lakini kwa masharti
– Mshindi alitakiwa kuelezea namna angetumia KSh30,000 na pia kuwachangia wasiojiweza
– Emmanuel Onu ndiye aliibuka mshindi baada ya kuorodhesha nyimbo zote za Akothee
Msanii mashuhuri wa KenyaAkothee, amemzawadi mmoja wa wafuasi wake mkubwa kwenye YouTube na KSh30,000.
Mwimbaji huyo mnamo Jumatatu, Desemba 30, aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kuwa anawazawadi wafuasi wake bora wa You Tube mwaka huu lakini kwa masharti ya kumwambia namna watatumia pesa hizo.
Akothee pia alitambua kuwa angependa sana endapo mshindi atatumia kiasi cha pesa hizo katika kuwasaidia wasiojiweza.
“Muda usiokuwa mrefu nitamzawadi mshindi wa YouTube, swali langu kwa mshindi wa KSh30,000 utakayopokea kutoka kwangu hii leo, uko tayari kuchangisha kiasi kwa wasiojiweza? Utatujulisha endapo utatajwa, hauhitaji kuwa milionea kupeana,” alisema Akothee.
Wafuasi wake walisongamana kwenye ukurasa wake huku wakiomba kupata pesa hizo kutimiza mahitaji yao na kazi za kutoa msaada katika jamii lakini Emmannuel Onu ndiye alimfurahisha Akothee kwa kuorodhesha nyimbo zake zote.
Mwanamuziki huyo alimtangaza Onu kama mshindi wa kinyanganyiro hicho na kumuomba kumtumia akaunti yake ya benki na nambari yake ya Mpesa.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.