Connect with us

General News

Binamu ya Uhuru amkosoa kuhusu kuidhinisha Raila – Taifa Leo

Published

on

[ad_1]

Binamu ya Uhuru amkosoa kuhusu kuidhinisha Raila – Taifa Leo

Binamu ya Uhuru amkosoa kuhusu kuidhinisha Raila

NA MWANGI MUIRURI

BINAMUYE Rais Uhuru Kenyatta amemkosoa kiongozi wa taifa akisema hatua yake ya kumuunga mkono Raila Odinga kuwa mrithi wake ni “kinyume cha kiapo kilicholishwa watu wa jamii ya Gema mnamo 1969”.

Bw Kung’u Muigai anasema waliokula kiapo hicho waliapa kuzuia babake Bw Odinga, Oginga Odinga na uzao wake kuchuka madaraka ya kuongoza Kenya.

Bw Kung’u alisema waliokula kiapo hicho wanapasa kutakaswa kabla ya kumuunga mkono Bw Odinga, la sivyo jamii ya Mlima Kenya ‘itapatwa na laana’.Alieleza kuwa uamuzi wa Rais Kenyatta kumuunga mkono Bw Odinga sio wa familia yote ya Kenyatta, mbali ni wake kama mtu binafsi.