Connect with us

General News

Duale akosa kunusurika shoka la Uhuru na habari zingine zenye gumzo.

Published

on

Duale akosa kunusurika shoka la Uhuru na habari zingine zenye gumzo.

Kila siku ya wiki, TUKO.co.ke inakupakulia kwa mukhtasari matukio na habari muhimu zilizogonga vichwa vya habari wiki hii ili ukapate kufahamu kwa upana na utendeti mambo yalivyo ulimwenguni.

Gavana Anne Mumbi Waiguru Jumatano, Juni 24, aliambia kamati teule ya seneti kuwa alitimuliwa kwa sababu ya kuunga mkono ripoti ya BBI.

Waiguru alisema hakuna ushahidi ambao uliwasilishwa mbeleya kamati hiyo na kwa hivyo ni siasa za kitaifa.

Habari

Waiguru alipofika mbele ya kamati ya Seneti. Picha: UGC.
Source: Facebook

Runinga ya K24 ambayo inamilikiwa na shirika la utangazaji la Media Max imewafuta kazi ghafla wafanyakazi zaidi ya 100.

Mtangazaji Nancy Onyancha pamoja na mumewe Joab Mwaura ambao walikuwa wakifanya kazi katika shirika hilo ni miongoni mwa wale waliopigwa kalamu.

Habari

Nancy Onyancha na mumewe Joab Mwaura.Picha: Nancy Onyancha.
Source: UGC

Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru aliwashangaza Wakenya mitandaoni baada ya picha kadhaa kuenezwa zikimuonyesha akishiriki mchezo wa kadi almaarufu ‘Solitaire’ kwenye simu yake.

Waiguru alikuwa akicheza mchezo huo wakati kesi dhidi yake ya kumfurusha mamlakani ilipokuwa ikisikizwa katika bunge la seneti.

Habari

Waiguru anaswa kwenye picha akichezo mchezo wa solitaire.Picha: The Star.
Source: UGC

4. Jalang’o aondoka Milele FM

Mcheshi Felix Odiwuor maarufu kama Jalang’o amejiuzulu kutoka kazi yake ya kifahari ya Milele FM.

Jalang’o alitangaza haya kupitia kurasa zake mtandaoni Jumatatu, Juni 22.

Mwanasiasa mkongwe, Nazlin Umar ameonekana kufurahia kung’olewa kwa Aden Duale kama Kiongozi wa Wengi Bunge la Kitaifa.

Umar, ambaye awali penyenye zilidai kwamba alikuwa katika uhusiano wa mapenzi na Duale, alishindwa kuficha bashasha yake kufuatia masaibu ya Duale.

Habari

Picha ya Dan Duale na Nazlin Umar. Picha: UGC.
Source: UGC

Mbunge wa Garissa Mjini Aden Duale alondolewa katika wadhifa wa Kiongozi wa Wengi Bungeni na nafasi hiyo kukabidhiwa Mbunge wa Kipipiri Amos Kimunya.

Habari

Aden Duale alitwaliwa na Mbunge Amos Kimunya.
Source: UGC

Aliyekuwa waziri wa Kilimo Mwangi Kiunjuri amesajili chama chake cha kisiasa tayari kwa mirindimo ya 2022.

Kulingana na kaimu msajili wa vyama Ann Nderitu, Kiunjuri amesajili chama cha The Service Party.

Habari

Mwangi Kiunjuri amekuwa akionekana kuwa mwandani wa Naibu Rais William Ruto kwenye siasa za 2022. Picha: William Ruto.
Source: UGC

Mwanamziki Betty Bayo Jumapili, Juni 21 aliwasisimua wanamtandao baada ya kumtumia aliyekuwa mumewe mhubiri Victor Kanyari ujumbe wenye utani siku ya kusherekea kina baba.

Vituko vya Gavana Waiguru Seneti na habari zingine zilizotamba wiki hii

Betty Bayo alimtumia aliyekuwa mumewe ujumbe wenye utani siku ya kusherekea kina baba.
Source: UGC

Comments

comments

Facebook

Trending