Connect with us

General News

Mbunge aomba wahisani wawasaidie wakazi na chakula – Taifa Leo

Published

on

[ad_1]

Mbunge aomba wahisani wawasaidie wakazi na chakula – Taifa Leo

Njaa: Mbunge aomba wahisani wawasaidie wakazi na chakula

Na MAUREEN ONGALA

MBUNGE wa Magarini, Bw Michael Kingi, ametoa wito kwa wahisani kusaidia wakazi wa Kilifi wanaoendelea kukumbwa na njaa.

Bw Kingi alisema chakula cha msaada kutoka serikali kuu na ile ya kaunti hakitoshi idadi kubwa ya wakazi ambao wameathirika.Alisema hayo alipoungana na kampuni ya Kensalt kutoa msaada wa bidhaa za chakula kwa wakazi wa eneobunge hilo.