[ad_1]
Kiongozi wa upinzani nchini Malawi Lazarus Chakwera aliibuka mshindi baada ya uchaguzi mkuu kurudiwa Jumanne, Juni 23
Chakwera alipinga matokeo ya uchaguzi wa awali akidai haukuwa wa haki na huru.
Baada ya uchaguzi kurudiwa, Chakwera alimshinda aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Peter Mutharika kwa kuzoa asilimia 58.57% ya jumla ya kura zilizopigwa.
Viongozi kadhaa akiwemo Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli wamempongeza Chakwera kwa ushindi huo.
Kupitia kwenye mtandao wa Twitter, Magufuli alisema nchi hizo mbili zitaendelea kuwa na uhusiano mwema kama awali.
“Nakupongeza Dkt. Lazarus Chakwera kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Malawi. Kwa niaba ya Serikali na Watanzania wote naahidi kuendeleza uhusiano wetu wa kidugu, kirafiki na ujirani mwema hususani katika masuala ya uchumi na ustawi wa jamii. Hongera sana Mhe. Rais.,” Magufuli alisema.
Chakwera aliaapishwa rasmi kuingia madarakani Jumapili, Juni 28, ambapo pia aliwashukuru wananchi wa Malawi kwa kumchagua kuwaongoza.
[ad_2]
Source link