Connect with us

General News

Jinsi ya kuandaa mishikaki ya maini – Taifa Leo

Published

on

[ad_1]

Jinsi ya kuandaa mishikaki ya maini – Taifa Leo

Jinsi ya kuandaa mishikaki ya maini

 

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 10

Muda wa mapishi: Dakika 20

Walaji: 4

Vinavyohitajika

maini kilo 1

tangawizi vijiko 2

pilipili kiasi

kitunguu saumu kijiko 1

chumvi kiasi

ndimu vijiko 2 vya chakula

beef masala kijiko cha chakula

karoti 1

mafuta kikombe ¼

Maelekezo

Osha maini vizuri.

Kata maini kwa urefu kisha kata vipande vikubwa kiasi

Jitahidi usikate vipande vidogo kwa sababu mishikaki ukiichoma ina kawaida ya kusinyaa (inakuwa midogo baada ya kuiva).

Weka viungo vilivyotajwa hapo juu isipokuwa mafuta na karoti.

Weka kwenye jokovu kwa muda wa saa moja au zaidi ili ipate kulainika. Ukiitoa ichanganye vizuri.

Katakata karoti kwa umbo la duara.

Chukua vijiti vya mishikaki, weka maini matatu yaachanishwe na karoti.

Weka jikoni kwa ajili ya kuioka kwa kutumia ovena ila unaweza kutumia jiko lolote.

Panga kwenye kifaa cha kuchomea kisha tumia brashi kupaka mafuta mishikaki yako.

Weka moto wa nyuzijoto 150 kwa kipimo cha sentigredi, moto wa juu na chini. Oka kwa dakika 20.

Kisha igeuze huku ukipaka mafuta tena oka kwa dakika 15 tu.

Hakikisha hauipiki kwa muda mrefu hadi ikakauka na kukakamaa.

Pakua na ufurahie na chochote kama slesi za mkate, wali na kadhalika.

[ad_2]

Source link

Comments

comments

Facebook

Trending