Connect with us

General News

Familia kupeana watoto kwa yeyote, yadai maisha imekuwa ngumu

Published

on

 

Jamaa mmoja pamoja na mkewe katika kijiji cha Kiaruhiu kaunti ya Nyeri waamua kupeana watoto wao kwa yeyote yule kwa madai ya kushindwa kukimu gharama za malezi

Samuel Ndung’u na mkewe Mary Nyambura wamemtaka msamaria mema ajitokeze ili awachukue watoto wao wawili awalee.

Familia Nyeri yajitolea kupeana watoto kwa yeyote, yadai kushindwa kukimu gharama za malezi

Ndung’ u anasema maisha yamekuwa magumu na ghali hata hawezi akawanunulia watoto wao chakula wala mavazi.
Source: UGC

Ndung’ u anasema maisha yamekuwa magumu na ghali hata hawezi akawanunulia watoto wao chakula wala mavazi.

” Nilifikiria maisha itakuwa mzuri lakini imenilemea, matajiri wengine ambao nafanyia vibarua wananidharau sana hasa wakijua unaishi maisha ya ufukara, kwa kweli mimi nimelemewa na niko tayari kupeana watoto wangu kwa yeyote yule ambaye yuko tayari kuwalea,” Ndung’u aliambia NTV.

Familia Nyeri yajitolea kupeana watoto kwa yeyote, yadai kushindwa kukimu gharama za malezi

Ndung’ u anasema maisha yamekuwa magumu na ghali hata hawezi akawanunulia watoto wao chakula wala mavazi.
Source: UGC

Mama wa watoto hao wawili wenye umri wa miaka miwili na miezi kumi mtawaliwa alisema hana budi ila kuwaona watoto wake wakiwa na maisha bora licha ya mdogo wake kuwa bado ananyonya.

Majiriani wao pia wamethibitisha kuwa familia hiyo inaishi kwa ufukara, malazi pia hawana na sasa wanaonelea wamefika mwisho wa maisha.

Comments

comments

Facebook

Trending