– Waziri Magoha amesema vijana wengi hutizama video za ngono kwenye mitandao ya kijamii na ndio sababu kuu mimba za mapema zinaripotiwa
– Magoha amesema atamshawishi Rais Uhuru Kenyatta aweke sheria zitakazozuia sinema zote zinazohusisha ngono
-Aidha, Magoha ameahidi kukabiliana vilivyo na wanaume watakaopatikana wakiwanyanyasa kijinsia watoto wa kike
Waziri wa Elimu George Magoha ametaka sinema za ngono zifutiliwe mbali kwenye mitandao ya kijamii hapa Kenya.
Magoha alisema kuwa sinema hizo ndicho kichocheo kikubwa cha mimba za mapema miongoni mwa wasichana haswa wenye umri wa chini ya miaka 19.

Waziri Magoha ametaka video za ngono mitandaoni zipigwe marufuku Kenya akidai zinachochea mimba za mapema
Source: UGC
Akizungumza akiwa mjini Nakuru Alhamisi, Juni 18, Magoha alisema atamshawishi rais Uhuru Kenyatta pamoja na mawaziri wenzake wazingatie kubadilisha sheria ili izuia sinema zote zinazohusisha ngono.
” Unaeza kuwa hauwazi kuhusu ngono lakini mtu anapofungua mitandao na kuanza kutizama video chafu, unaanza kufikiria vinginevyo, mbona hizi sinema sinakubaliwa Kenya?, sisi hatuzihitaji,” Magoha alisema.

Magoha alisema kuwa sinema hizo ndicho kichocheo kikubwa cha mimba za mapema miongoni mwa wasichana haswa wenye umri wa chini ya miaka 19.
Source: Facebook
” Sio eti lazima ziwe Kenya kwa sababu Marekani zipo, kuna nchi kadhaa Afrika ambazo zimepiga marufuku tuvuti zinazoonyesha video hizo,” Magoha aliongezea.
Hata hivyo, Magoha alitilia shaka madai kuwa idadi kubwa ya wasichana waliochini ya umri wa miaka 19 wamepachikwa mimba kati ya Januari na Mei mwaka huu.
” Nitachunguza madai kuwa idadi kubwa ya wasichana wa shule wamepachikwa mimba, jambo hili ni lakusikitisha sana, mimi kama profesa najiuliza, hawa wasichana waliripoti wapi kuwa wamepata mimba?, nani anatoa twakimu hizi?, hazikai za kuaminika,” Magoha alisema
Aidha, Magoha ameahidi kukabiliana vilivyo na wanaume watakaopatikana wakiwanyanyasa kijinsia watoto wa kike.