[ad_1]
Meidi anunulia mwajiri bahili nyama kilo tano
MURANG,A MJINI
Na MIRIAM MUTUNGA
KIJAKAZI wa hapa, alishangaza mdosi wake alipoenda sokoni na kununua nyama ya kilo tano na kuandalia familia yake baada ya kupatiwa mshahara wake.
Inasemekana demu alifanya hivyo kwa kuwa mke wa mdosi alikuwa akimnyima nyama. “Leo nimewaandalia chakula kitamu sana ambacho tangu nilipoajiriwa hapa sijawahi kula,” kijakazi alisema. Mdosi alitabasamu na kumsifu demu huyo kwa lengo ya kumkashfu mke.
“Kweli. Hiki ni chakula kitamu mno. Mungu akubariki sana,” mume wa mdosi alisema huku akimtazama mkewe kwa jicho jeuri. Inasemekana mama wa nyumba aliumwa sana kufuatia tabia yake ya kunyima mwanadada nyama, akaomba msamaha na kuahidi kubadilika.
[ad_2]
Source link