Rapa Jackson Makini almaarufu Prezzo amekiri kuwa hatawahi msahau aliyekuwa mpenzi wake wa zamani mtangazaji na mwanamuziki Sheila Mwanyigha ama kwa majina ya usanii Nikki
Prezzo alifichua kuwa Nikki alisimama naye wakati alimhitaji sana na kwa mawazo yake hakujua kwamba angeweza kumuokoa kwa lolote.
Akizungumza kwenye mahojiano na CTA, Prezzo alielezea jinsi alivyomnasua kutoka mikononi mwa maafisa wa polisi baada ya kupatikana na silaha kule Sarit Centre.
Prezzo alikamatwa na maafisa wa polisi na kutupwa katika kituo cha polisi cha Parklands, alijaribu kwapigia simu watu kadhaa akiwemo mjombake simu lakini hakupata usaidizi wowote.
Wazo lilimkujia la kumpigia Nikki simu, alipofika kituoni, mambo yakawa nywee kwani alimtumia mamake ambaye alikuwa afisa mkuu katika kituo hicho kumuondoa kwenye seli.
” Nikki alikuwa mtu wa mwisho kumpigia simu, sikujua kwamba angeniokoa, alifika akiwa ameniletea juisi na machungwa,” Alisema Prezzo.
” Amini usiamini, ni yeye aliniondoa kweny seli kupitia kwa mamake ambaye kwa wakati huo alikuwa afisa mkuu wa polisi katika kituo cha Parklands, mamake aliamru niondolewe makosa yote na niachiliwe huru, kwa hili jambo, sitawahi msahau Nikki ila nitaishi nikimshukuru,” Aliongezea Prezzo.
Prezzo na Nikki walichumbiana kwa miaka kadhaa kabla ya kuachana, uhusiano wao ulikuwa tamanio kwa wengi.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.